Friday, February 19, 2010

Huyo ndiye ROONEY!


Wayne Rooney ni mpachika magoli maarufu kwa sasa wa timu ya soka ya Manchester United ya Uingereza ni mchezaji anayependa soka na kulicheza kwa kiwango cha juu kabisa. Awapo uwanjani Rooney hujituma sana katika kupachika magoli si mtu wa kumwacha pekee hata kidogo ni hatari kwa timu pinzani.

Akitolewa nje na kocha wake huwa anakuwa na ghadhabu isiyosemeka. Rooney anawea kupiga ngumi ukuta, anaweza kuvua gloves na kuzibwaga chini au kufanya lolote lile. Lakini utampenda akifunga goli. Husheherekea kwa mbwembwe zote unazozifahamu anaweza kuserereka kwa magoti bila kujali kuchubuka. Pichani Rooney (mwenye glovu nyeusi) akipongezwa na wachezaji wenzake baada ya kufunga goli.

No comments: