Thursday, February 11, 2010

Sioni sababu ya Prof.Maghembe kujiuzulu watoto wetu hawasomi

Binafsi, matokeo ya mtihani wa kidato cha IV mwaka 2009 kwa idadi kubwa ya watahiniwa kushindwa hayakunishangaza sana. Nilitegemea hivyo kwani watoto wetu hawapendi kujifunza. Tatizo si vitabu, si walimu si kiingereza. Mbona hata hicho kiswahili ndo wameshindwa vibaya. Lugha wanayoitumia kila siku. Kwenye shule hizo hizo za kata kuna waliopata division I na II.

Idadi kubwa ya wanafunzi katika shule zetu za sekondari ni sababu ya msingi kwa wanafunzi kufanya vibaya. Njia za kuwachuja wanafunzi hawa kabla ya kufanya mtihani wa kidato cha nne zimeondolewa. Kulikuwa na mtihani wa kidato cha pili, sasa hauko unategemea nini? Si wanakwenda waliokuwemo na wasiokuwemo ili mradi kafika kidato cha IV.

Huwezi kulinganisha na mfumo wa elimu kwa shule za seminari za kikristu. Kule wanafunzi huchujwa kwelikweli kiasi kwamba yule anayebahatika kufika kidato cha nne hawezi kukosa Division 4 chunguza kwa makini utagundua hilo.

Kitu cha kufanya sasa ni kwamba wazazi, walimu na wizara husika tujipange kuhakikisha kuwa watoto wetu wanasoma. vinginevyo takwimu hizi zitazidi kuwa mbaya mwaka hadi mwaka. Kwahiyo wale wanaopiga kelele kuwa Prof.Maghembe ajiuzulu naona hawamtetendei haki.

No comments: