Friday, February 19, 2010

Magufuli anatuambia nini kuhusu utafiti wa kuku wa asili?


Katika Taarifa ya mafanikio ya miaka minne ya serikali ya awamu ya nne. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akielezea mafanikio yaliyopatikana kutoka utafiti wa kuku wa asili ni kwamba kuku wa asili anapopewa chakula cha ziada badala ya kujitafutia chakula wao wenyewe; utoaji wa mayai unaongezeka kutoka wastani wa mayai 10 hadi kufikia kati ya mayai 18 hadi 25 kwa mtago. Ukuaji wa vifaranga unaongezeka kutoka wastani wa gramu kati ya 3 hadi 5 hadi kufikia wastani wa gramu 8 na 10 kwa siku. Kiwango hiki cha ukuaji kinaonyesha kuwa kuku anaweza kufikia kati ya kilo 1.5 hadi kilo 2 kwa kipindi cha miezi 6 tu. Aidha kuachisha makinda/vifaranga ndani ya wiki 4 kunaongeza idadi ya mitago kutoka kwa wastani 2-3 kwa mwaka hadi wastani wa mitago 6 - kwa kolowa kwa mwaka na hivyo kuongeza idadi ya mayai kutoka wastani wa mayai 40-60 hadi 90-120 kwa kolowa kwa mwaka. Matokeo haya ni mazuri ni ni changamoto kwa wafugaji. Nyama ya kuku wa asili ni tamu sana tujitahidi kufuga.

No comments: