Friday, February 19, 2010

Vyakula dawa vinavyorefusha maisha



Leo katika pekuapekua yangu nimekuta kilichotayarishwa na Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika kinachoelezea vyakula dawa vinavyorefusha maisha kwa wanaoishi na virusi vya UKIMWI.

Vyakula hivyo ni Viungo (husaidia kutuliza au kutibu matatizo ya afya kama kutapika, kuharisha, mafua, kichefuchefu na kujaa gesi tumboni. Mboga na Matunda ni chanzo cha vitamini na madini muhimu mwilini husaidi kuongeza damu, uzito na vitamini A . Mimea kama ubuyu wenye vitamini C hutuliza mafua na kuongeza hamu ya kula, choya (rozela) husaidia pia kuongeza damu. Shubiri (alovera) husaidia kutibu magonjwa mbalimbali yakiwemo malaria na kisukari. Kipeperushi hicho kinapatiokana kupitia barua pepe: psk@kilimo.go.tz

No comments: