Tuesday, February 2, 2010

Nazi zimeanza kuadimika Dar


Wali ulioungwa kwa nazi ni chakula kitamu sana lakini ni cha gharama. Kiungo cha nazi kimeanza kuwa adimu siku hizi jijini Dar. Si rahisi kwa sasa kwa watu wenye kipato cha chini kutumia kiungo hicho. Bei ya nazi jijini Dar ni kati ya Tzs 500-1000/- kwa nazi. Inasemekana kuwa nazi nyingi zinasafirishwa kwenda nchini Comoro. Juhudi zifanyike zakuweza kuongeza uzalishaji wa nazi kwani ni kiungo kinachopendwa na wengi na madhara yake kiafya ni kidogo.

No comments: