Thursday, February 11, 2010

Hivi tunasafisha nyumba zetu tunapotembelewa na wageni?

Juma la jana wakati wa kuadhimisha miaka 33 ya CCM Mwenyekiti wa chama hicho Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete alikuwa na ratiba ya kutembelea wana CCM katika jiji la Dar Es Salaam. Kilichotokea kila sehemu walijitayarisha kwa kila hali. Wakazi wa Mbagala walishuhudia mitaro ya maji kutengenezwa na kusafishwa kwenye barabara ya Kilwa. Uchafu wa siku nyingi ulifanyiwa kazi kwa siku mbili tatu tu. Haya ndiyo maisha yetu. Tunasafisha nyumba zetu pale tu wageni wanapotutembelea si kwa usafi wetu. Tunataka watu watuone tu wasafi wakati ukweli ni kwamba tunaishi kwenye uchafu daima.

No comments: