Tuesday, February 16, 2010

Tutaukumbuka Mradi wa Minazi


Tanzania tuna bahati kubwa sana ya kustawisha mazao ya aina mbalimbali katika ekolojia tofauti. Kwa kuwa tuna bahari kuna mazao yanayostawi ukanda wa pwani. Kwa kuwa tuna sehemu za nyanda za juu tuna mazao yanayostawi huko kama vile ngano pamoja na matunda ya nchi zenye baridi za ulaya.

Nazi ni zao linalostawi sehemu nyingi hapa nchini lakini kwa miaka ya hivi karibuni upatikanaji wake umekuwa ni wa shida sana hata kusababisha bei ya nazi pamoja na madafu kupanda kwa haraka sana. Uzalishaji wake umeshuka kwa kuwa minazi mingi hukatwa kupisha makazi ya watu hasa sehemu za Pwani. Vilevile magonjwa yamesababisha minazi mingi kusinyaa hivyo kushusha uzalishaji.

Zao la nazi miaka ya 80 hadi 90 lilikuwa likishughulikiwa sana na Mradi wa Kitaifa wa Kuendeleza Zao la Mnazi (National Coconut Development Project-NCDP). Mradi huu ulifanya kazi kubwa licha ya dosari ndogo ndogo zilizojitokeza baada ya kumalizika kwa mradi hasa kwa mbegu fupi kutokubaliwa na wakulima wengi baada ya kuona kuwa huchakaa baada ya muda mfupi.

Hali ikiendelea hivi bila kuchukua hatua madhubuti uzalishaji wa nazi utashuka mwaka hadi mwaka na madafu nayo yataadimika na be itapanda sana.

No comments: