Thursday, July 29, 2010

Bakhresa na kiwanda cha matunda Mwandege

Kiwanda kipya cha kusindika matunda cha Bakhresa kimeanza kufanya kazi katika eneo la Mwandege wilaya ya Mkuranga kilometa chache kutoka Kongowe mkoa wa Dar Es Salaam.Kiwanda hiki kwa hakika ni mkombozi kwa wakulima wa matunda hapa nchini hasa wa mikoa ya Pwani, Dar Es Salaam, Morogoro na Tanga ambako kunazalishwa aina mbalimbali za matunda. Huu ni fursa ya pekee kwa wakulima kuongeza uzalishaji wa matunda kwani soko lipo. Kwa habari ambazo si rasmi zinasema kuwa kiwanda hicho hutayarisha juisi nzito na kuyahifadhi katika magudulia makubwa kabla ya kupeleka Vingunguti kwa ajili ya kutengeneza juisi laini tayari kwa matumizi.Kiwanda hiki kimeanza kutoa ajira kwa watanzania.

No comments: