Thursday, July 1, 2010

HUREE MWAKA MPYA!


Leo tarehe 1/7/2010. Serikali inaanza mwaka mpya wa 2010/11. Mwaka huu tutegemea mambo mapya mengi tu. Uchaguzi wa kuingoza serikali ya Jamhuri ya Tanzania unafanyika mwaka huu kwa hiyo matarajio ya wengi ni makubwa.Hata hivyo dalili za bajeti zinaonyesha kuwa tutajifunga mikanda zaidi kwa bidhaa kupanda bei. Hali ya maisha ya wananchi wa kawaida kwa kweli itakuwa si nzuri. Lakini kama tutatekeleza vizuri mipango tuliyoipanga katika kila sekta mambo yatakuwa shwari.

No comments: