Thursday, July 22, 2010

Kama mambo yenyewe hivi STAR MEDIA mtafulia


MWEZI wa tano mwaka huu nilinunua king'amuzi kutoka kampuni ya STAR MEDIA(Tanzania) kwenye kituo chao cha Buguruni kwa lengo la kupata chaneli nyingi kupitia luninga yangu. Kilichonivutia zaidi ni bei nafuu pamoja na antena ambayo siyo lazima uwe na dish.

Tatizo linakuja pale unapoongeza muda wa matumizi kwa kutumia vocha zao. Maelezo yanayotolewa kwa kweli ni magumu.Binafsi napata shida kuweza kupata huduma za chaneli kupitia king'amuzi hicho.

Wale akina dada waliopo vituoni Buguruni na Ukonga hawajui kumuhudumia mteja. Tahadhari nawapa msiporekebisha hali hii wateja tutawakimbia sasa hivi oh!

No comments: