Thursday, July 29, 2010

Chuma-Banzi-Luanda wanapokutana

Siku ya tarehe 25/07/2010 marafiki wa siku nyingi yaani Banzi, Chuma na Luanda tulikutana pale Msimbazi Centre. Ni kipi kilichotukutanisha? - 'Lukemo lwa Lusona' (mwito wa ngoma). Aliyetoa mwito ni nani? Ni Bwana Michael Luanda.

Sisi watatu ni marafiki wa siku nyingi. Sote tumesoma Shule ya Msingi Matombo miaka ya mwanzo wa sabini.Sote kwa kipindi fulani tumeishi Kigogo! Isitoshe mimi na Luanda tumeenda Sekondari ya Njombe mwaka 1974. Sasa Luanda anaozesha shemeji yake. Ametuita tushirikiane kwa hilo.Tulipokutana tulikumbuka mambo mengi. Msalabani, solono za mtoni mfizigo,Kiswira Sports Club na hatukukosa kugusia mbunge mtarajiwa wa Morogoro kusini!

No comments: