Friday, July 30, 2010

Yapo maharage yaliyotafitiwa


KAMA ilivyo kwa mahindi.Kaya nyingi hapa nchini hutumia maharage kwa mboga. Ni ukweli usiofichika kuwa kama unampata mpishi mzuri akakupikia maharage kwa nazi na akaunga wali kwa nazi hakika hutaacha kula chakula hicho. Watafiti wetu wameshafanya utafiti na wanaendelea kufanya utafiti wa aina mbalimbali za maharage. Kuna maharage ya rojorojo kuna maharage yanayopendwa kwa rangi yake na hata yale yanayostawishwa kwa ajili ya kusindika au kula yakiwa machanga. Waulize watafiti wa kutoka Selian Arusha na Uyole Mbeya utapata jibu na kuanza kustawisha maharage au kula maharage au kufanya biashara ya maharage.

No comments: