Thursday, July 29, 2010

Kilimo cha Miti na Mazao-Agroforestry


AGROFORESTRY-Kilimo cha Miti na Mazao (Tafsiri yangu). Wengi hutafasiri kuwa ni Kilimo Mseto ambapo mimi sikubaliani nao. Kwani mseto ni mchanganyiko. Tuachane na habari ya tafsiri tuangalie faida ya Kilimo cha Miti na Mazao. Pamoja na kutunza mazingira, kilimo hicho kinatusaidia katika kuwa na kipato mbadala kwa vipindi tofauti mwaka mzima. Unaweza kuvuna mbao,matunda,asali,nafaka,mboga na mazao jamii ya mikunde. Kilimo hiki kinapaswa kuendelezwa hapa nchini kutokana na hali halisi ya mazingira tuliyo nayo.

No comments: