Tuesday, July 20, 2010

Tujipange vizuri tuongeze uzalishaji katika kilimo


Hebu angalia pichani baadhi ya mazao yanayostawi hapa Tanzania kuna ndizi,muhogo,mtama,zabibu.kabichi,viazi vitamu,maharage,ngano,mpunga,alizeti,mahindi na mbaazi. Hivi kweli nchi hii ni ya kulia njaa? Ni kwanini wananchi wake bado ni masikini? Ni vizuri wote tukajipanga na kupeana muda wa utekelezaji wa uzalishaji wa mazao mbalimbali kwa kiasi kinachohitajiwa na ubora unaotakiwa. Kilimo Kwanza isiwe maneno tu tushiriki sote.

No comments: