Tuesday, December 29, 2009

Dawasco bomba linavuja kituo cha Msikiti-Kilwa Road

Leo asubuhi wakati nikija kazini karibu kabisa ya kituo cha Msikiti mara baada ya kumaliza makaburi ya Mbagala Mission tulikuta maji ya kitiririka barabarani yakiashiria kuvuja kwa bomba. Hatari ni kwamba hali hiyo isipodhibitiwa haraka maji yatachimba barabara na hivyo magari kukwepa shimo hilo hatimaye kusababisha msongamano wa magari pengine hata ajali ndiyo maana nawakumbusha DAWASCO wafanye hima kurekebisha hali hiyo.

No comments: