Sunday, December 13, 2009

Kutemewa mate ni dharau

Mtu anapokutumea mate ni dharau. Huyu Mkanada aliyemtemea mate askari wetu wa barabarani pamoja na mwandishi wetu wa habari Jerry Muro amefanya dharau kubwa kwa nchi hii. Kwa maoni yangu wazungu walio wengi wanatudharau sana sisi waafrika hata ukitembelea nchi zao utaona kabisa dharau machoni mwao. Kama kicheko basi ni cha kejeri. Pamoja na kuwa aliyefanya kitendo hicho ni mfanyakazi wa balozi hiyo, naomba serikali yetu iwe na msimamo kwa hili wasituchezee.

No comments: