Wednesday, December 16, 2009

Kwanini Benki Kuu?


Leo hii kuna habari nyeti kwenye gazeti la Rai Mwema Desemba 16-Desemba 22,2009 inayosema "Ulaji wa Vigogo wa BoT wahojiwa." Ninachohoji mimi ni kwanini wafanyakazi wa Benki Kuu wanapewa kipaumbele katika maslahi? Mishahara yao ni ya Juu. Bado wanapewa motisha wa kukopa kiasi kikubwa cha fedha. Na inawezekana kabisa bila riba. Ikiwa mfanyakazi wa chini kiwango cha kukopa ni milioni 30 Mungu akupe nini. Kuna haja gani ya kusoma hesabu au fizikia nchi hii ikiwa kwa kuwa muhudumu wa ofisi tu Benki unalipwa mshahara mkubwa kuliko Mhandisi au Bwanashamba?

Hivi karibuni Rais Jakaya Mrisho Kikwete alitoa agizo kwa watafiti wa sekta ya kilimo kuongezewa mishahara yao kutokana na kazi nzuri wanayoifanya katika sekta hiyo. Hadi leo agizo halijatekelezwa. Kwa hali hii nani afanye kazi sekta ya kilimo. Watoto wetu watakimbilia sekta nyingine hasa za fedha. Tuangalie hili. Picha kushoto Prof.Beno Ndulu, Gavana wa Benki Kuu Tanzania.

No comments: