Friday, December 18, 2009

Naambiwa hiki ni kijiji cha China


Miaka takribani ishirini iliyopita China ilikuwa ikidharaulika sana. Labda ilikuwa ikiogopwa kwa wingi wa watu wake na umahiri wao kwenye vita. Lakini nchi za magharibi iliiponda sana hasa kutokana na siasa yake Ujamaa.

Lakini sasa ni tishio. Waamerika wanaigwaya China. Kitu gani ambacho China hawawezi kukifanya. China wamebakia kuwa wajamaa huku wakiboresha maisha ya wananchi wao. Hebu angalia picha kushoto kwako, hicho ni kijiji mojawapo kilichopo China. Wanapanga na kutekeleza haya ndiyo maendeleo tunayotaka. Ubepari sawa lakini kwa faida ya nani? Ubepari huku tunashindwa kuzibua mitaro ya maji machafu? Ubepari huku tukishindwa kupaka rangi hata majengo ya umma?Ubepari wakati makao makuu ya nchi umeme kwa mgao?

3 comments:

Sir Gabriel sos Limbe said...

NENDA

Innocent John Banzi said...

Iko siku nitaitembelea CHINA

Sir Gabriel sos Limbe said...

kWELI FANYA HIVYO USI AMINI TUU...BORA KUDANGANYWA (JAPO SIPENDI)-KULIKO-KUJIDANGANYA