Wednesday, December 16, 2009

TUACHE MALUMBANO YASIYO NA MSINGI TUJENGE NCHI

Kwa muda mrefu sasa kumekuwa na malumbano yasiyo kwisha kwa viongozi wa vyama vya siasa wakituhumiana kama watoto wadogo. Huyu akimwambia mwenzake hana elimu, mwingine akimweleza mwenzie hana busara. Na hawa wote ni watu wakubwa kwenye vyama vyao. Wakati wananchi wengine wakihangaika jinsi ya kupata riziki tena kwa shida kubwa. Wakubwa hawa wako kwenye malumbano tena kwa faida yao. Watoto wetu wanapata elimu duni, hospitali za umma bado ni dhaifu kwa huduma zinazotolewa, miundo mbinu bado ni duni. Wananchi wananyonywa vibaya kupitia simu za mkononi, miji yetu ni michafu hasa Dar.Tuache malumbano tujenge nchi yetu.

No comments: