Wednesday, December 16, 2009

Jamani eh Maximo kichwa ngumu tuachane naye


Karibu miaka mitano sasa. Sioni la kushangaza kutoka kwa Maximo kwa timu yetu ya Soka ya Taifa. Nionacho mimi ni kutuchanganya tu. Tunaishi kwa matumaini kuwa iko siku. Siku iko wapi wakati kila siku anaunda timu ya Taifa. Kocha mwenye kinyongo kwa baadhi ya wachezaji, kocha asiyejua lugha yetu ya Taifa kweli huyu ni kocha? Tuachane naye. Kiasi anacholipwa Maximo hata kama nusu yake angalipwa Mziray, Kibadeni, Mkwasa, au Kayuni timu ingefanya vizuri tu. Timu inapata misaad ya nguvu kutoka kwa NMB, Serengeti na wadau wengine lakini upangaji mbovu wa timu ndo unaoiua Taifa na Kilimanjaro Stars

No comments: