Tuesday, December 29, 2009

Mifereji ya barabara ya Kilwa isilipuliwe

Kuna zoezi linalokwenda kwa kasi la kujenga mifereji kwenye barabara ya Kilwa. Naambiwa kuwa hilo lilikuwa ni agizo la Mhe. Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aliyeagiza mamlaka husika kushughulikia mifereji hiyo haraka iwezekanavyo kuepusha hatari ya kuharibika barabara mpya iliyojengwa. Ninachoona mimi ni kuwa mifereji hiyo inajengwa haraka lakini si kwa kiwango kinachotakiwa. Ni kweli wajenzi ni wazawa. Lakini uzawa isiwe 'issue' ya kulipua kazi. Kwa maana nimeshaona baadhi ya maeneo mifereji imeshaanza kuchimbika kutokana na mvua hizi zinazonyeesha.

No comments: