Friday, December 18, 2009

Tuwasikilize wakulima kuhusu mfumo wa stakabadhi ghalani


Nimewasikia wakulima wakilalamika kuhusu mfumo wa kuuza mazao wa stakabadhi ghalani. Pengine wazo ni zuri lakini utaratibu uliopo wa kuwezesha mfumo huo kufanya kazi haujakaa sawa. Nikiwa kwenye gari dogo la abiria likitokea Mkuranga kwenda Mbagala Rangi tatu mama mmoja alikuwa akiulalamikia mfumo huo kwa zao la korosho. Fedha wanazolipwa mara tu wanapouza korosho ni kidogo aidha malipo yaliyosalia hayajulikani yatalipwa lini. Kwa maoni yake anaona heri korosho zao zingenunuliwa na wafanyabiashara wa kujitegemea kuliko vyama vya ushirika. Kwa hili tuwasikilize wakulima na penye dosari turekebishe.

No comments: