Friday, December 18, 2009

TUSIDHARAU KAULI WANAZOTOA VIONGOZI WA DINI


Hivi karibuni gazeti moja litolewalo kila siku hapa nchini liliandika kuwa "KILIMO KWANZA NI WIMBO TU" kauli hii imetolewa na Mhashamu Kardinali Polycarp Pengo kiongozi wa Wakatoliki hapa nchini.

Tulio wataalamu wa Kilimo tusibeze kauli hii eti kwa kuwa sisi na watu wa kilimo au kuona kuwa Pengo hakipi umuhimu KILIMO. Viongozi nan wataalamu tujiulize kipi kifanyike ili kweli KILIMO KIONEKANE KUWA KWANZA hapa nchini. Tuone mabadiliko kwenye sekta hiyo kuanzia kwenye kupanga raslimali na utekelezaji wake vinginevyo inawezekana kabisa kuwa WIMBO TU. Kwa maoni yangu huenda viongozi wa dini wako sahihi. Hawa wako karibu sana na wananchi na wananchi huwa huru kueleza hisia zao kwa viongozi wa dini.

No comments: