Friday, December 18, 2009

Ziara za mafunzo kwa wakulima


Moja ya urithi alioucha marehemu mama yangu ni doti ya Khanga iliyoandikwa "Tembea Uone" Ni kweli mimi mwenyewe nimetembea na kuona mengi na kujifunza mengi na kuacha mengi.

Tunapotaka wakulima wajifunze teknolojia mpya moja ya mbinu zinazotumika ni kuwapatia ziara za mafunzo. Bado tunaamini kuwa "Tembea uone." Kwenye ziara hizi wakulima huona na kujifunza haraka. Wanaweza kujifunza jinsi ya kufuga kuku kutoka kwa wakulima wenzao kwa mazingira yanayofanana na ya kwao, jinsi ya kulima aina fulani ya zao kama vile nyanya, vitunguu n.k. kwa ufanisi zaidi. Wanajifunza pia jinsi wakulima wanavyoweza kujenga nyumba nzuri kwa kutumia raslimali walizonazo. Wanaweza kujifunza pia kumbe hata mkulima wa embe anaweza kumiliki gari!
Ukiona huwezi kusahau kwa urahisi. Nahitimisha kwa kusema kuwa ziara za mafunzo kwa wakulima ni muhimu. Pichani wakulima wakiwa katika ziara ya mafunzo wakionyeshwa namna ya kuchota maji kwa ajili ya umwagiliaji toka kwenye kisima nyumbani kwake huko Ibumila Njombe.

No comments: