Sunday, December 13, 2009

Kipi kinachoitangaza Tanzania?

Elimu ya msingi, wanafunzi 50% hawakufaulu mtihani wa darasa la saba mwaka huu. Jiji la Dar Es Salaam ni chafu. Uzalishaji katika kilimo bado ni wa chini. Miundo mbinu ni ya ubabaishaji. Umeme si wa uhakika. Maji ni kwa mgao. Michezo- Mpira wa mguu timu ya Taifa haijafanikiwa kupata ushindi na kutwaa kikombe kwa muda mrefu. Madini ndo tunaambulia athari za kuharibika kwa mazingira pamojan na wananchi kupata vilema badala ya kuwa matajari. Hivi Tanzania ukiondoa amani na usalama tuna lipi la kujivunia. Hata usafi tu ni issue! Mwe!

No comments: