Tuesday, December 29, 2009

Garage za mtaa wa Mkumba-Wailes ni uchafu

Jana jioni wakati nikitoka kazini nilibahatika kupitia mtaa wa Mkumba uliopo Wailes-Temeke na kuona magari mabovu pande zote za barabara hiyo. Nilipojaribu kuuliza ni kwanini kuwepo kwa hali hiyo? Nikajibiwa aah mzee usishangae hizo ni garage za mitaani.

Hivi kweli watendaji wa Temeke mmerizika na hali hiyo? Jiji hili bado kunakuwa na garage za mitaani? Aah ondoeni uchafu huo haipendezi hata kidogo.

No comments: