Monday, December 28, 2009

RUZUKU IPIMWE KWA UZALISHAJI


Yapata miaka mitatu sasa tangu serikali ianze utaratibu wa kutoa ruzuku ya pembejeo hasa mbolea kwa wakulima hapa nchini. Ruzuku hii hutolewa kwa mfumo wa vocha. Mfumo huu wa ruzuku kwa kutumia vocha unakuwaje hasa. Hapa kichafanyika ni kwa serikali kugharamia asilimia fulani ya gharama za pembejeo kwa mfumo wa vocha hivyo kumpunguzia makali ya uzalishaji mkulima. Mfumo huu ulipoanza ulikumbana na matatizo mengi kila mwaka maboresho yamekuwa yakifanywa ili ruzuku iweze kutoa matokeo yanayokusudiwa. Mimi naamini kuwa matokeo mazuri yatapatikana kwa kuongezeka uzalishaji na kuleta tija kwa wakulima.

No comments: