Thursday, December 31, 2009

Kila kifo ni cha ghafula-Sheikh Yahya

Mapema leo asubuhi nilikuwa nikitazama kipindi cha Jambo Tanzania kinachorushwa na TBC. Mmoja wa wageni waliokaribishwa katika kipindi hicho ni Mnajimu wa siku nyingi Afrika Mashariki na Kati Sheikh Yahya ambaye hivi karibuni utabiri wake uliodai kuwa atakayegombea nafasi ya Rais katika uchaguzi wa mwakani kumpinga Rais wa sasa Mhe. Jakaya Kikwete atakufa ghafla. Akionyesha uhodari wa kujenga na kutetea utabiri wake na hoja hiyo alisema kuwa wanadamu tusiogope kifo kwani kinapotokea kina faida na hasara. Kwa mfano ni pale tu mzazi anapofariki ndipo watoto wanapopata fursa ya kurithi mali za mzazi.

No comments: