Saturday, September 15, 2012

Miaka 12 -Mwanafunzi wa Chuo Kikuu

Mtoto Xavier Gordon wa Uingereza akiwa na umri wa miaka 12 (pichani) amejiunga na Chuo Kikuu huko Uingereza. Inasemekana Xavier ndiye mwenye umri mdogo zaidi kuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu. Ingawa kwa sasa anaendelea na masomo yake ya darasa la nane lakini mara tatu kwa mwezi huhudhuria masomo katika Chuo Kikuu Huria huko East Grinstead Uingereza, tena masomo anayochukua kwenye shahada yake ni hesabu.Yeye hupendelea maeneo magumu ya hesabu kama vile 'abstract structures' Vector and calculus na Newtonian mechanics - tena kwa muda wake mwenyewe (kujisomea). Hata hivyo kulingana na umri wake wakati anapokwenda chuoni husindikizwa na watu wazima kwani bado ni mdogo.

No comments: