Monday, January 14, 2013

Mtaalamu shambani kwa mkulima

Afisa Kiungo wa Kanda (ZIELO) ya Kaskazini Bw. Jeremiah Sembosi hufanya kazi shambani na wakulima. Yeye ni kiungo kati ya wakulima watafiti na wagani. Huelezwa matatizo ya wakulima na kuyaweka katika lugha inayoeleweka ili watafiti wayapatie ufumbuzi. Hutambua teknolojia inayotakiwa na wakulima isambazwe na wagani.Hiyo ndiyo kazi ya Afisa Kiungo wa Kanda pamoja na Timu yake. Pichani anaonekena mkungu wa ndizi aina ya Williams na baadaye anaongea na mkulima Elizabeth akiwa na mumewe wakazi wa kitongoji cha Ngarenaro A, kijiji cha Endanoga, kata ya Gallapo wilayani Babati mkoani Manyara wakieleza mafanikio waliyoyapata kutokana na kilimo cha migomba ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba ya kisasa, kusomesha watoto wao na kuongeza miradi mingine ya ng'ombe wa maziwa na mbuzi wa maziwa

No comments: