Friday, January 11, 2013

Zahanati ya mimea bila jengo

"Niliposikia zahanati ya mimea niliwaza na kufikiri kuwa inahitaji mambo mengi sana na makubwa kumbe kinachohitajika ni daktari wa mimea na vifaa vyake,mwavuli, meza ndogo,na viti." Anabainisha Bw. Livingstone Mwedipando wa ARI-Selian, Arusha aliyetuma picha hii. Chini ya mwavuli huu, wakulima huleta sampuli za mimea yenye matatizo aidha magonjwa , wadudu na hata dalili za upungufu wa virutubisho. Daktari wa mimea hutoa huduma za kutambua na kushauri. Kwa njia hii daktari mmoja anao uwezo wa kuhudmia wakulima wengi kwa siku kulingana na mahitaji. Picha hii inaonyesha zahanati ya mimea iliyopo kwenye soko la Sadala wilayani Hai mkoani Kilimanjaro

1 comment:

Innocent John Banzi said...

Ha! Nilifikiri zahanaiti ni kwa wanadamu tu kumbe hata mimea?