Saturday, November 26, 2011

Tumsome Mshindo Msolla


Dr. Mshindo Msolla ni mmoja ya watu waliojaliwa vipaji hapa duniani. Yeye mtaalamu bingwa kwenye raslimali ya udongo. Aidha Msolla ni kocha mahiri wa mchezo wa mpira wa miguu (Soccer). Ameshawahi kufundisha timu ya Taifa mara nyingi katika vipindi tofauti. Kwa mapenzi aliyonayo kwenye soccer, Msolla ana mraba wake katika gazeti la 'The Citizen' kila Jumamosi. Mraba wake unaitwa 'Looking at Sports with a bird's eye' ndani ya mraba huo Msolla huchambua masuala mbalimbali yanayohusu michezo hapa nchini na duniani kwa jumla.Katika mraba wa leo, Msolla anakuja na rai ya vilabu vikubwa vya soka hapa nchini kukuza vipaji vya wanasoka vijana kwa kuwasajili katika ligi kuu badala ya kupoteza fedha nyingi kusajili wachezaji wazee waliokwisha kutoka nje. Swadakta! Dr. MSOLLA.

No comments: