Friday, November 21, 2014

Kutoka Bukoba hadi Bungeni Dodoma

Hivi ndivyo tunavyotakiwa kuwajenga watoto wetu wawe na uelewa mpana na kujenga uzalendo wa kuipenda nchi yetu. Wanafunzi hawa wa shule ya Rweikiza kutoka Bukoba wamesafiri hadi Dodoma kutembelea Bunge letu kujifunza jinsi Bunge linavyofanya kazi. Hivi kweli hawa wakipata swali linalouliza jinsi Bunge linavyofanya kazi watashindwa kulijibu? Hapa wanakutana na Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda. Ona jinsi Pinda alivyofurahi akizungumza nao. Shule zinatakiwa kuwa na programu za aina hii. Huwezi kuzungumzia Bunge la London wakati la kwenu la Dodoma hulifahamu!

No comments: