Tuesday, November 18, 2014

Vifaa ninavyotumia ofisini

Nilianza kuchukia mwandiko mbaya tangu nikiwa shule ya msingi, nilipenda kuiga mwandiko wa Mama Beatrice Mhango, shangazi Pauline Mloka, Baba yangu Mkubwa Mwl. Ephrem Ephrem Mbiki, Kaka Seraphin Chibby na marehemu uncle Longin Mizambwa hawa walinivutia kwa wakati huo na kwa kweli niliwaiga kwa kuumba herufi mojamoja niipendayo na kuchanganya na kutoka na mwandiko wangu 'unique'. Nilipofika sekondari pale Njombe niliwakuta wanafunzi wanaoandika miandiko mizuri sana akiwemo rafiki yangu marehemu John Makoroma (The Printer) wengine walionivuta kuandika mwandiko mzuri ni uncle Nestory Daulinge, uncle Balozi Daniel Mloka, rafiki  na wengine wengi walioandika vizuri. Kwa hali hiyo nilipenda pia kutumia kalamu nzuri ndiyo maana mpaka sasa moja ya vitu ninavyovipenda kuwa navyo katika maisha yangu ni kuwa na kalamu nzuri. Ingawa kuna kompyuta na ni mtumiaji mzuri lakini sikosi kununua kalamu nzuri hata fountain pens ninazo na si moja ni za aina aina. Angalia vifaa ninavyotumia kikazi na kwa mawasiliano ninavipenda na vinanipa motisha ya kuandika. Napenda kuandika katika maisha yangu napenda pia kutumia zana bora.

No comments: