Tuesday, November 18, 2014

Mbeya City Kwishneee

Kuna msemo wa Kiswahili unaosema kuwa, ngoma ikilia sana haikawia kupasuka. Hiki ndicho kilichotokea kwa timu ya soka ya Mbeya City. Msimu uliopita ilikuwa tishio kwa timu nyingine kila timu iliyotia mguu Mbeya ilifungwa au kutoka sare.Mwaka huu kinyume chake watu wanakwenda Mbeya wanajichukulia pointi kirahisi. Nasikia kisa ni ukata. Mwaka wa jana timu ikishinda kila mchezaji alipata posho ya shilingi 25,000/= na sare 15,000/= mwaka huu mpango huo haupo. Nimesoma hivi karibuni kwenye gazeti moja hapa nchini kuwa kocha wa timu hiyo Bw. Mwambusi 'amebwaga manyanga.' Sijui ni kweli.

No comments: