Wednesday, October 19, 2011

Kambare na Kitoga


Kamabare na Kitoga ni aina ya samaki wapatikanao kwenye maji baridi. Si rahisi sana kuwatofautisha wanapokuwa wakubwa hasa wakipasuliwa.Hatan hivyo wengi tunawatambua kambare wadogo waliokaushwa na kukunjwa mikia yao ikitafuna midomo na vichwa vya vikubwa vyenye sharubu. Lakini pia minofu ya kambare ina miiba midogo midogo mingi tofauti ya Kitoga. Wengine husema pia kambare ana shombo! Vinginevyo wote ni samaki wa tamu ingawa mimi napenda zaidi Kitoga. Pichani darajani Ruvu Kambare na Kitoga wakiwa sokoni.

No comments: