Tuesday, October 11, 2011

Watafiti waandamizi


Kutoka kushoto kwenda kulia Mary Lutkamu (Mkurugenzi Msaidizi Utafiti-Special Programme), Dr.Mary Shetto (Afisa Utafiti Kilimo Mkuu),Eva Kanyeka (Afisa Utafiti Kilimo Mkuu)baadhi ya wataalamu watafiti waliopo Makao Makuu ya Idara ya Utafiti na Maendeleo, Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika wakiandaa taarifa kwa pamoja ofisini kwa Mkurugenzi leo asubuhi. Nami nilishiriki kwenye jopo hilo la wataalamu. Ilituchukua takribani masaa 4 kuweka sawa taarifa ya awali ya mafanikio ya utafiti miaka 50 ya UHURU.Hatukwenda Hotelini hivyo ilibidi tupate chai humo humo ofisini huku kazi ikiendelea. Katika mazingira haya bajeti ya vitafunwa ni muhimu! Bi Rose Angelo msaidizi wa Ofisi alituhudumia.

No comments: