Wednesday, July 16, 2014

India - hakuna kulala utafiti wa Bioteknolojia








Utafiti wa Biteknolojia umepiga hatua kubwa nchini India. Hapa kuna Centre ya Biotechnology Research. Bioteknolojia ni muhimu kwa wakati tulionao sasa kwasababu matatizo yanayoikumba sekta ya kilimo katika uzalishaji ni mengi kama vile visumbufu vya mimea na maabadiliko ya hali ya hewa ambapo baadhi yake utafiti wa kutumia njia za kawaida umeshindwa kuleta majibu yanayotakiwa.Kwa kutumia bioteknolojia imewezekana. India imewekeza  vya kutosha katika utafiti huu. Wana watafiti mahiri  na miundo mbinu ya kisasa. Tulipotembelea centre hiyo, tuliwakuta  watafiti vijana wanaume kwa wanawake wakiendelea na utafiti kwa ari. Hii imebainika kutokana na uwezo wao wa kujieleza pamoja na taarifa za kitafiti walizokwishazitoa.

No comments: