Friday, July 11, 2014

India wanao wakulima wa mfano











India  ina wakulima wengi wa mfano. Mmoja wao ni huyo mwenye shati la mistari  (bluu,nyeupe na nyeusi) ambaye tulipata bahati ya kumtembelea. Ni mkulima kijana kutoka Gurgaon.Ana eneo la shamba lipatalo eka 50 ambalo analima mazao hasa ya matunda. Ana mifugo (ng'ombe na nyati) ambao mmoja wa ng'ombe wake hutoa lita 30 kwa siku. Mkulima huyu  anashirikiana na wataalamu wa kilimo kutoka 'Farmers' Science Centre' kwa kuzitumia teknolojia zinazobuniwa na watafiti kwenda kwa wakulima kwa lengo la kuboresha uzalishaji. Shamba lake hilo la matunda ambalo linamwagiliwa maji hupata asilimia 90 kutoka serikalini kumsaidia kuimarisha miundo mbinu ya umwagiliaji shambani.

No comments: