Wednesday, July 16, 2014

Utafiti wa Post Harvest -Technology- India



Tunaweza kuzalisha mazao mengi tukashindwa kuyatumia au kuyahifadhi kwa matumizi ya baadaye. Badala ya kula maembe,machungwa, mananasi au ndizi kama tunda, mpunga kama wali, mahindi na muhogo kama ugali, tunaweza kusindika na kupatabidhaa nyingine kama vile  juice,pombe, biskuti,maandazi,mikate n.k. Bidhaa hizi zinaweza kuuzwa kwa bei nzuri kuliko zinapouzwa kama matunda au nafaka. Isitoshe kama tutajenga viwanda vya kutengeneza bidhaa hizo kama afanyavyo Bakhresa, wananchi watapata ajira. Hivyo kuna haja ya kujenga uwezo wa 'Post harvest research' katika vituo vyetu vya Utafiti kama walivyofikia wenzetu Wahindi. Katika Taasisi ya Utafiti wa Kilimo India, watafiti wamefanya kazi kubwa katika eneo hili na hivyo kuwa na ushirikiano na viwanda katika kuzalisha bidhaa hizo kwa wengi kwa ajili ya matumizi kwa walaji hivyo kuongeza kipato cha wakulima na kuboresha maisha yao,lishe ya wananchi na kukuza uchumi wa taifa

No comments: