Friday, May 14, 2010

Aza ya mbegu ya mazao ya mizizi


Picha hii nimeinyaka kutoka blog ya kaka Mjengwa. Wadau hawa wamekusanya mbegu ya viazi vitamu. Tatizo la mbegu za mazao ya mizizi ni kubwa hapa nchini hata wakala wa mbegu - ASA ulioanzishwa hivi karibuni bado haujapata ufumbuzi wa kuzalisha mbegu bora za mazao ya mizizi-viazi vitamu ikiwa mojawapo.

Kwa kuwa mazao ya mizizi (hasa muhogo na viazi) hustahimili sana ukame hivyo kuwa mkombozi wakati wa njaa, juhudi lazima zifanyike kuhakikisha kuwa wakulima wanapata mbegu bora na za uhakika. Hapo ndipo Halmashauri zinapotakiwa kutenga fedha za kutosha kuwawezesha wakulima kupata mbegu.

No comments: