Thursday, May 27, 2010

Machiavelli na werevu

"Kuna aina tatu za werevu.Wa Kwanza hutambua mambo yalivyo wao wenyewe. Wa pili hutambua mambo yalivyo kupitia kwa wengine. Wa tatu hawatambui mambo yalivyo si kwa kupitia wao wenyewe bali pia kwa wengine. Werevu wa kwanza ni mzuri zaidi, wa pili ni mzuri kiasi; lakini wa tatu ni hovyo na hauna manufaa."

Maneno hayo yalitamkwa na mwanafalsafa wa kale wa Italia, Nicolo Machiavelli. Alizaliwa Mei 3,1469 huko Florence, Italia na kufariki Juni 21,1527 huko Florence. Moja ya vitabu vyake vilivyopata umaarufu duniani ni The Prince (1513). Tafakari hii.

No comments: