Thursday, May 13, 2010

Daraja la UMOJA-kumbe tunaweza


Ujenzi wa Daraja la Umoja lililojengwa kwa ushirikiano wa nchi mbili za Tanzania na Msumbiji zimedhihirisha kuwa Afrika tunaweza kufanya mambo makubwa yanayoweza kuwasaidia watu wetu bila kusubiri wafadhili. Daraja hilo lenye urefu wa mita takribani 750 na thamani ya zaidi yaTzs 36 bln limefunguliwa rasmi jana tarehe 12/5/2010 ni mfano mzuri wa ushirikiano wa kuigwa barani Afrika. Daraja hili linawaunganisha si wa Msumbiji na Tanzania tu bali watu wote. Limerahisisha usafiri, litakuza shughuli za biashara, litapunguza vifo kwa wale waliokuwa wakisafiri kwa vyombo visivyovyakuaminika kuvuka mto Ruvuma na hatimaye kupata ajali. Kubwa zaidi litaboresha maisha ya wananchi wa nchi zote mbili.

No comments: