Wednesday, May 19, 2010

Bango hili limepoteza maana


Wengi wetu hupenda kutumia lugha ya Kiingereza wakati tunapotangaza jambo lakini kwa bahati mbaya lugha hiyo wengi imetutupa mkono. Lakini inashangaza inapofikia wakati mfanyabiashara kuridhika kutangaza biashara yake kwa lugha ambayo haielweki. Hebu soma kilichoandikwa kwenye bango hilo pichani - 'BLANTAYA GROOCARE'.

Wakati nikisoma makala hii iliyoandikwa na mwana mraba Abdi Sultani katika mraba wake maarufu ujulikanao ' Our Kind of English' unaolimwa kila siku ya Jumapili katika gazeti la SUNDAY CITIZEN kumbe bango hilo linamaanisha BLANTYRE GROCERY. Blantyre ni mji wa biashara wa Malawi na Grocery ni mahali ambapo kinywaji (pombe) inapatikana kwa tafsiri ya Tanzania. Picha hii imepigwa huko Nachingwea - Kilimalondo Road. Tuwe makini katika lugha ya kiingereza.

No comments: