Friday, May 28, 2010

Mmea wa Sale kwa Wachagga



Kwa wale waliokwisha kubahatika kufika mkoani Kilimanjaro, natumaini wameshawahi kuuona mmea unaoonekana pichani. Mmea huu unaitwa Sale. Je, una thamani gani kwa Wachagga?

Wachagga wanaamini kuwa Sale ni mkombozi wa jamii. Mmea wa Sale hutumika kwaajili ya kuweka mipaka katika mashamba yao ili kuweza kujua eneo la mtu mmoja na mwingine.

Matumizi mengine ya sale ni katika masuala ya ndoa na mahusiano.Kwa Wachagga, kuna aina moja ya kuoa ambayo ni ya mkato isiyofuata taratibu ambazo zimezoeleka katika jamii nyingi. Kijana wa Kichagga anaweza kuelewana na masichana bila ya kuomba ridhaa ya wazazi. Kielelezo cha ndoa hii ni jani la mmea huo.

Aidha, mmea huo hutumika katika utatuzi wa migogoro kwa kuomba radhi na wahusika hukaa na kusameheana. Anayetumwa kusuluhisha mgogoro huchukua mmea wa sale. Haya ndiyo matumizi makuu matatu ya mmea wa sale kwa Wachagga (Habari hii imefupishwa kutoka Gazeti la Mwananchi la tarehe 28/05/2010)

No comments: