Friday, May 7, 2010

Ukitegemea huwezi kuendelea


Huu ndiyo ujumbe aliyoutoa Rais wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Benjamin William Mkapa (pichani). Mkapa alisema "inashangaza zaidi, kukuta viongozi wa Afrika wanazungumzia maendeleo ya nchi zao, lakini mnauliza ni nani atampa fedha; ni wapi tutapata na wala si kuazima, huu ni ugonjwa." Huu ni ukweli hata katika ngazi ya familia. Ikiwa wewe na familia yako maisha yenu ni kutegemea wengine hamwezi kuendelea na maisha yenu yatakuwa ya shida. Kibaya zaidi mtakuwa hamna maamuzi katika maisha yenu. Hebu mcheki Mkapa ndani ya suti ya 4 buttons babake bonge la tai kweli anapendeza.

No comments: