Friday, May 14, 2010

Saini na SAHIHI

Neno saini limetokana na 'sign' ambalo ni Kiingereza.Tumelikopa na kulitohoa ili lifanane na muundo wa Kiswahili na liwe ni neno kamili la Kiswahili. Linaweza kutumika kama kitenzi na pia kama nomino.

Saini (kitenzi) kutoa idhini ili kitendo fulani kitendeke au kipatikane. Matumizi yaliyozoeleka na kukubaliwa na wengi ni kutoa idhini au kuthibitisha kupatikana kwa kitu au jambo fulani na mara nyingine ni kwa kuandika jina lako.

Tunatumia neno hili tunapotaka kuweka saini mahali fulani. Ni sahihi kusema kuweka saini na wala siyo kutia saini. Kutia lina maana ya kufanya kitu kiwemo ndani ya kitu kwa mfano nitilie chai badala ya kusema niwekee chai. Kuweka kitu maana yake ni kukitua kama vile kuweka kitabu mezani au kuweka silaha chini.

Neno sahihi (nomino) lina maana ya kuthibitisha au kuidhinisha kwa jambo kutendeka au kupatikana. Tumezoea kusema, "Kazi aliyofanya ni sahihi. Pia, maswali yote aliyajibu kwa usahihi kwa maana ameyajibu yote sawasawa."

No comments: