Wednesday, May 19, 2010

Kwetu Mbagala


Wilaya ya Temeke imejaliwa kutoa wasanii wenye vipaji katika soka na muziki. Kwenye anga za mziki kuna vijana wa TMK walikotoka Juma Nature na Mheshimiwa Temba. Hivi majuzi tu ameibuka msainii mwingine kwa jina Naseeb Abdul a.k.a. Diamond alisomba tuzo tatu kwa mpigo 'hat trick' kwenye tuzo za Kilimanjaro. Huyo ndiye aliyeimba kwetu Mbagala. Nakupa shavu Diamond mimi kwetu Kisemvule na mji wetu mkuu Mbagala. Kuna nini tena umekata ngebe mwanangu! Pichani Diamond akifurahia moja ya Tuzo yake.

No comments: