Wednesday, May 5, 2010

Gharama za kupanda miti aina ya minazi barabara ya Sam Nujoma ni ipi?

Gazeti la Daily News la tarehe 5/5/2010 limeandika habari moja kwenye kurasa za mbele inayohusu Dar Es Salaam inavyooteshwa miti katika jitihada za kupamba jiji tayari kwa mkutano wa Kimataifa utakauzungumzia masuala ya uchumi. Kilichonishtua ni gharama za kuotesha miti hiyo je ni Tzs 700,000/- kwa mti mmoja au US $ 700,000 . Haikuelezwa wazi wazi. Au gharama za kuotesha miti 50 ni Tzs 700,000/- au US $ 700,000. Kama kuna aliyeisoma habari hiyo basi anieleweshe.

No comments: