Saturday, May 22, 2010

Wizi wa mafuta ya Tansforma


Wizi wa mafuta ya transforma unatokea mara kwa mara hapa nchini. Wiki iliyopita umetokea sehemu ninayoishi mimi - Kisemvule, wilaya ya Mkuranga, Mkoa wa Pwani. Vijana wamekuja usiku wameweka mpira na kunyonya mafuta hayo. Matokeo yake ilipofika muda wa saa 1.00 asubuhi transforma ililipuka na hadi hivi sasa kijiji giza totoro hatuna umeme. Visima vya maji vilivyokuwa vikitumia umeme kupump maji havifanyi kazi, hakuna kuona TV. Wanafunzi katika shule za bweni wameaathirika kwa kuwa watapata shida kukamilisha home work zao.

Ndugu zangu Wazaramo waliopanga kuwa na 'shughuli' mambo yameharibika. Ndo maana nilipoona picha hii ya gari la TANESCO niliyoikuta kwenye blog ya Mjengwa ilibidi niiandikie stori hii.

Eti mafuta hayo yanatumiwa kukaangia chips matone machache yakichanganywa na mafuta ya kukaangia basi hayakauki! Nasikia pia mafuta hayo hutumiwa na wezi kwa kubomolea nyumba, yakimwaga ukutani, ukuta humomg'onyoka hivyo kuwa rahisi kuingia ndani. Aidha wengine husema hutumiwa kwenye pump za maji, wengine husema hutumiwa katika utengenezaji wa vipodozi vya akina mama waonekane 'wazungu'!

No comments: